Saturday, 11 March 2017

Chirwa, Msuva kupeleka maumivu Zanaco leo


KOCHA wa Yanga, George Lwandamina, amesema hakuna kitakacho wazuia leo kupata ushindi kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa Afrika huku akiamini washambuliaji wake, Simon Msuva na Obbrey Chirwa watapeleka kilio kwa wapinzani wao Zanaco.

Yanga inacheza na Zanaco leo kwenye Uwanja wa Taifa kuanzia saa 10:00 jioni ukiwa ni mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Msuva na Chirwa wamekuwa kwenye kiwango cha juu huku wakiisaidia Yanga kupata ushindi kwenye michezo yao.

Wiki iliyopita Chirwa alionyesha kiwango cha juu kwenye mchezo wa kombe la FA dhidi ya Kiluvya United na kufunga magoli manne katika ushindi wa bao 6-1 waliupata Yanga.

Msuva, anayeongoza kwenye orodha ya wafungaji kwenye ligi kuu msimu huu akiwa na magoli 12, amekuwa na mchango mkubwa kwenye kikosi cha Yanga na leo anatagemewa kupeleka kilio kwa Wazambia hao.

Akizungumza na gazeti hili jana, Lwandamina, alisema kuwa hana hofu na mchezo wa leo kwa kuwa kila kitu amekiweka sawa na kazi imebaki kwa wachezaji wake tu.

"Naamini kwa kile tulichokifanya mazoezini na kama wachezaji watafuata maelekezo yangu, nina uhakika wa ushindi mzuri kesho (leo)," alisema Lwandamina.

Alisema kuwa anawafahamu wapinzani wao wa leo kwa kuwa amekutana nao mara kwa mara kwenye Ligi ya Zambia wakati alipokuwa akiifundisha Zesco ya nchini humo.

Lwandamina, alisema watacheza soka la kushambulia muda wote na kujaribu kuwabana wapinzani wao wasitengeneze nafasi ya kupata bao litakalovuruga mipango yao.

Mchezo wa leo utachezeshwa na mwamuzi Aden Abdi kutoka Djibout akisaidiwa na Hassan Yacin na Farhan Salime.

Wakati Yanga wakicheza leo Uwanja wa Taifa, wawakilishi wengine wa Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho, Azam FC watashuka Uwanja kesho kuumana na Mbabane Swallows kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Mchezo huo wa hatua ya kwanza umepangwa kuanza saa 1:15 usiku.Chirwa, Msuva kupeleka maumivu Zanaco leoChirwa, Msuva kupeleka maumivu Zanaco leo


Simba uwanjani Dodoma leo

KATIKA kujiimarisha kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, vinara wa ligi hiyo, Simba leo watashuka kuwakabili Polisi Dodoma katika mchezo wa kirafiki utakaofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani humo.

Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, aliomba mechi hiyo ya kirafiki ili kuwafanya wachezaji wake waendelee kuwa na 'joto' la mashindano wakati michezo ya Ligi Kuu Bara imesimama kwa muda.

Omog alisema kuwa kwake mechi ya leo anaipa uzito kwa sababu anataka kuona wachezaji wake wanashinda na kuwafurahisha pia mashabiki wa timu hiyo wa mkoa huo.

"Ni mechi ya kirafiki, lakini kiufundi tunaiangalia kwa jicho lile lile linalofanana na pale tunapocheza na Yanga, hatutaki kupoteza mechi yoyote kuanzia sasa hadi mwisho wa msimu huu," alisema Omog.

Kocha huyo wa zamani wa Azam FC aliongeza kuwa licha ya kuwa na majeruhi, amewataka wachezaji watakaopata nafasi ya kucheza kuonyesha uwezo wao na kuwania namba katika kikosi cha kwanza.

"Hii ni timu, mchezaji atakayecheza vizuri atanishawishi kumpanga katika kikosi cha kwanza au kusubiri kwenye orodha ya wachezaji 18, kuna baadhi ni wazuri wakianza au wakiingia baada ya kuwasoma wapinzani," Omog aliongeza.

Baada ya mechi ya leo, Simba inatarajiwa kuelekea Tabora kucheza mechi nyingine ya kirafiki huku Jumapili ikitua Arusha kuwakabili wenyeji Madini FC katika mchezo wa hatua ya robo fainali ya mashindano ya Kombe la FA.

Mimba zakatisha masomo wasichana 48


WASICHANA 48 katika shule za msingi na sekondari wilayani Karagwe mkoani Kagera, wameacha shule kutokana na sababu mbalimbali, ikiwamo mimba.

Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe, Adeodata Peter, alisema wanafunzi 25 walipata mimba, wanne waliolewa na tisa walitoroshwa na kuacha masomo kwa mwaka 2016.

Adeodata alibainisha kwamba halmashauri hiyo imewachukulia hatua mbalimbali za kusheria wanaume wote waliohusika kuwapa mimba wanafunzi hao.

Kwa mujibu wa Adeodata, miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kufungua mashtaka na mpaka sasa baadhi yao wameshtakiwa na kuhukumimwa.

Hata hivyo, Adeodata hakufanya zaidi kuhusu adhabu za zilizotolewa na mahakama ukiwamo muda wa vifungo.

Hata hivyo, aliongeza kuwa zipo hatua kadhaa zinazoendelea kuchukuliwa katika halmashauri za kukabiliana na matukio hayo.

Miongoni hatua hizo, Adeodata alisema kuwa ni Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe inaimarisha idara ya jinsia na watoto na kuwezesha wasichana kutekeleza majukumu yao kwa jamii.www.omblox.blogspot.com

Viroba vya mil. 130/- vyakamatwa


MSAKO wa kukamata pombe kali aina za viroba mkoani Dodoma umeshika kasi, baada ya Jeshi la Polisi kukamata shehena yenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 134.9.

Polisi walikamata shehena hiyo ya viroba kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA) na Mamlaka ya Mapato Tanzani (TRA).

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Lazaro Mambosasa, alisema walikamata katoni 2,199 katika wilaya za Dodoma na Mpwapwa zenye thamani ya Sh. 134,954,500.

“Huo ni mwendelezo wa oparesheni ya kutekeleza agizo la Serikali la kukamata wauzaji, wasambazaji, na watumiaji wa pombe iliopo katika vifungashio vya plastiki maarufu kwa jina la viroba ambayo imepigwa marufuku tokea Machi Mosi mwaka huu,” alisema Mambosasa.

Aliwataja waliokamatwa na bidhaa hiyo kuwa ni mkazi wa Area C, Consolata Mallya (58) kutoka kampuni ya Cowike Enterprises LTD, ambaye alikutwa na viroba Original na katoni 421, na Zed 1248.

Wengine ni mkazi wa Mpwapwa, Jobu Timoth, ambaye alikutwa na viroba katoni 62.5 na Siloya Mbonyi, wa kampuni ya Takawedo ambaye alikutwa na katoni 444.

Aliwataka wafanya biashara wa dawa za kulevya kuacha mara moja biashara hiyo kwa sababu sio halali.Viroba vya mil. 130/- vyakamatwa

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salam, limetangaza vita dhidi ya matapeli mitandaoni ambao wamekuwa wakitumia jina la mke wa rais mstaafu Salma Kikwete na Mwenyekiti wa IPP, Dk. Reginald Mengi, na kujipatia mamilioni ya fedha kutoka kwa wananchi.

KAMISHNA SIMON SIRRO.
Kamanda wa Kanda hiyo, Kamishna Simon Sirro, alisema matapeli hao wamekuwa wakitumia jina la Salma Kikwete, Dk. Mengi na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, kuwatapeli wananchi.

Alisema wamekuwa wakiwahadaa wananchi watume Sh. milioni moja ili wakopeshwe Sh. milioni 10 na bajaji moja mpya.

Sirro alisema baadhi ya matapeli hao ambao wameshakamatwa, wamekuwa wakifanya utapeli huo kupitia taasisi feki ya ‘Focus Vicoba’ iliyopo kwenye mtandao wa Facebook.

“Kuna uwapo wa taasisi feki ya fedha yenye jina la Focus Vicoba kwenye mtandao wa Facebook na tovuti inayojulikana kwa jina la www.vicobaloanstz.wapka-mob ambayo hutumia majina ya viongozi serikalini na watu maarufu kutapeli,” alisema.

Alisema majina ya viongozi hao yamekuwa yakitumika kufungua akaunti za Facebook na tovuti mbalimbali ambazo matapeli hao hutumia kuwarubuni watu kwamba wanaweza kupata mikopo yenye masharti nafuu na haraka kwa njia ya mtandao.

“Katika ufuatiliaji wa suala hili kitengo cha upelelezi wa makosa ya mtandao cha polisi Kanda Maalumu, kimebaini katika tovuti hiyo picha na jina la Mama Salma limetumika na kwenye ukurasa wa Facebook linatumika jina la Dk. Mengi.

“Wanatumia majina pamoja na namba za simu 0757 308 381 na 0768 199 359 ambazo sio namba za Mama Salma wala Dk. Mengi,” alisema.

Kamanda Sirro alisema ufuatiliaji uliofanyika Desemba 16, mwaka jana uliwezesha kumkamata mtu mmoja (jina tunalo) ambaye kwa sasa ana kesi mahakamani.

Sirro alitoa onyo kwa wale wanaoendelea kufanya udanganyifu na kujipatia fedha kwa njia isiyo halali kupitia mitandao ya kijamii, waache mara moja.

Lema achokoza mapya Arusha


Lema achokoza mapya Arusha
MBUNGE wa Arusha Mjini Godbelss Lema, amechokoza mapya jijini Arusha, kwa kuwapandisha jukwaani wanaye wawili na kudai kama kushtakiwa kwa amri ya polisi iliyomtaka awe mzungumzaji pekee katika mkutano wa hadhara, basi waunganishwe wote na kushakiwa.

Lema alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika shule ya Msingi Ngerenaro kwa ajili ya kusalimiana na wananchi pamoja na wapigakura wake, baada ya kuachiwa na mahakama kwa dhamana wiki iliyopita.

Katika barua ya polisi ya kumruhusu kufanya mkutano jana, walimtaka kuwa mzungumzaji pekee katika mkutano huo, lakini Lema akasema amewapandisha jukwaani watoto hao ili kama kumshtaki basi waunganishwe wote.

Baada ya kupandishwa jukwaani, Lema aliwaita watoto wake (Briliant na Terence) ambao waliwasalimia wananchi kwa nyakati tofauti kwa salamu za Chadema wakianza kwa kuzungusha ngumi na kutamka People’s.

Wakati wakisalimia wananchi, watoto hao kila mmoja kwa wakati wake waliimba wimbo wa ‘CCM kwisha, kwisha kabisa. Mbende mbende, nyang’a nyang’a…kifo cha mende, chalii; hakuna kulala mpaka kieleweke,’ na kuwafanya mamia ya watu waliokuja kusikiliza mkutano huo kuangua kicheko