Saturday, 11 March 2017
Lema achokoza mapya Arusha
Lema achokoza mapya Arusha
MBUNGE wa Arusha Mjini Godbelss Lema, amechokoza mapya jijini Arusha, kwa kuwapandisha jukwaani wanaye wawili na kudai kama kushtakiwa kwa amri ya polisi iliyomtaka awe mzungumzaji pekee katika mkutano wa hadhara, basi waunganishwe wote na kushakiwa.
Lema alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika shule ya Msingi Ngerenaro kwa ajili ya kusalimiana na wananchi pamoja na wapigakura wake, baada ya kuachiwa na mahakama kwa dhamana wiki iliyopita.
Katika barua ya polisi ya kumruhusu kufanya mkutano jana, walimtaka kuwa mzungumzaji pekee katika mkutano huo, lakini Lema akasema amewapandisha jukwaani watoto hao ili kama kumshtaki basi waunganishwe wote.
Baada ya kupandishwa jukwaani, Lema aliwaita watoto wake (Briliant na Terence) ambao waliwasalimia wananchi kwa nyakati tofauti kwa salamu za Chadema wakianza kwa kuzungusha ngumi na kutamka People’s.
Wakati wakisalimia wananchi, watoto hao kila mmoja kwa wakati wake waliimba wimbo wa ‘CCM kwisha, kwisha kabisa. Mbende mbende, nyang’a nyang’a…kifo cha mende, chalii; hakuna kulala mpaka kieleweke,’ na kuwafanya mamia ya watu waliokuja kusikiliza mkutano huo kuangua kicheko
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment
Phone: +255745767927
Email: jeremiahelijah01@gmail.com
facebook page: OMBLOX